March 2026

Matangazo ya usharika tarehe 29 Machi 2026

DAYOSISI YA MASHARIKI NA PWANI

MATANGAZO YA USHARIKA

 TAREHE 29 MACHI, 2026

SIKU YA BWANA YA MWISHO KABLA YA PASAKA

(PALMARUM-SIKU YA MITENDE)

 NENO LINALOTUONGOZA NI:

“NDIYE MBARIKIWA AJAYE KWA JINA LA BWANA”

1. Tunawakaribisha wote tumwabudu Mungu wetu katika Roho na kweli.

2. Wageni: Hakuna mgeni aliyetufikia na cheti.

3. Matoleo ya Tarehe 22/03/2026

Jumla - Tshs 22,787,500/= +USD 9,153/=+SA RAND 10,+DIRHAM 5

MATOLEO KATIKATI YA WIKI

Azania Front Yaadhimisha Siku ya Wanawake Duniani 2026

Siku ya Jumapili, Machi 8, 2026 ilifanyika ibada ya kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani katika Usharika wa Kanisa Kuu Azania Front. Ibada za aina hii hufanyika kila Jumapili ya kwanza ya mwezi Machi kila mwaka ili kutoa fursa kwa wanawake kuongoza matukio na huduma zote za ibada. 

Ibada zote tatu za siku hiyo ziliongozwa na wanawake ambapo neno kuu la siku hiyo lilikuwa ni kuwakumbusha wanawake na washarika wote Kutunza Mazingira.